Jumanne, 22 Oktoba 2019

KUNA SIRI ILIYOFICHIKA KATIKA VITABU


Kama vile ambavyo kuna siri katika kupata utajiri,kuwa na ndoa bora;vivyo hivyo kuna siri kubwa iliyojificha katika vitabu.
Jamii imekuwa na mwamko mdogo wa usomaji wa vitabu kwa sababu kadha wa kadha.Lakini sababu mojawapo ambayo inachagiza jamii isiwe na mwamko wa kusoma vitabu imejikita katika tamaduni.
Tamaduni zetu zimeathiri usomaji wa vitabu kuwa duni,Hii inatokana jamii imejikita kushugulika na shughuli za kijamii zaidi kama vile kulima ,kucheza ngoma n.k.
Tunaona asilimia kubwa ya wateja wengi wa maktaba zetu ni wanafunzi na wanavyuo , pia inatoka na kundi hili wanasoma vitabu iwasaidie katika kujibia mitihani yao.

Kwa nini vitabu vimebeba siri?

Kwanza, Kitabu kinafanya msomaji kuwa mbunifu na kupata maarifa mengi yatakayomsaidia  kufikia katika maendeleo ya hali ya juu.Kwa hiyo tunaweza kusema kuna faida kubwa kwa jamii kujijengea tabia ya kusoma vitabu ni chanzo cha kupata maendeleo.

Pili,Kitabu kinasaidia kujenga jamii inayo heshimu haki za binadamu.Tunaona kwa sasa nchi nyingi zinapambana na raia wake kuheshimu haki za binadamu.Nahamini kupitia siri iliyojificha kwenye kitabu itasaidia jamii kuwa utu na kuwajali watu wengine itapunguza visa vinavyotokea vya uvunjifu wa haki za binadamu.

Naomba nihitimishe makala hii kwa kuwahimiza wanajamii kujenga tabia ya kusoma vitabu ili kusaidia jamii zetu ikue kimaendeleo.



Jackson C. Chacha
Lushoto,Tanzania
22/10/2019

Jumamosi, 6 Aprili 2019

KUJENGA JAMII YENYE UELEWA NA HUDUMA ZA KIUKUTUBI

Awali ya yote nitumie ukurasa huu kuwashukuru nyote mnaopitia ukurasa huu kwa ajili ya kujifunza na kupata elimu zinazohusu huduma za Maktaba.karibu sana.
Naomba nianze moja kwa moja kwa kuleta ufafanuzi wa mada tajwa hapo juu.

MKUTUBI ni Nani?
Kwa kweli hili neno linaweza kuwa geni masikioni mwa watu wengi ila ndiyo ukuaji wa kiswahili ulivyo ila itoshe kusema Mkutubi ni mtu mwenye weledi wa taaluma ya maktaba na kazi yake kubwa ni kuweka mpangilio mzuri wa machapisho yote yaliyopo ndani ya maktaba ili kumrahisishia msomaji kupata machapisho kwa urahisi.

Baada ya kufahamu dhana nzima ya neno "Mkutubi" tuangalie lengo la mada yetu.

Kwa ujumla maktaba ni mkusanyiko wa machapisho mbalimbali yaliyopangiliwa kwa usahihi kumrahisishia msomaji aweze kupata hitaji lake kwa muda sahihi.
Maktaba haiwezi kukamilisha kazi zake bila kuwepo Mkutubi aliyepata mafunzo/elimu ya kutosha ya kiukutubi ,ambayo itaweza kukamilisha maana nzima ya uwepo wa huduma ya maktaba.

Jamii ina wajibu wa kuelewa huduma za maktaba ili kuwa na taifa lenye watu walioelemika,hivyo ni jukumu la serikali kuongeza nguvu zaidi kwenye kujenga miundombinu ya kutosha hasa sehemu za pembezoni zizofikika huduma za maktaba kupanua wigo kwa jamii kuelimika.