Jumamosi, 13 Mei 2023

MAKTABA MTANDAO

 Maktaba mtandao linaweza kuwa jina geni kwa baadhi yetu,lakini tusishangazwe na jina unajua kiswahili ni lugha pana sana hasa kwa dhama hizi za ukuaji wa Sayansi na Teknolojia.

Maktaba Mtandao ni neno ambalo limetafsiriwa kutoka lugha ya kiingereza likiwa na maana ya "digital library".

Nini maana ya Maktaba Mtandao?

Maktaba Mtandao ni mkusanyika wa machapisho mbalimbali yaliyopangwa kwa mifumo maalumu na kuhifadhiwa kwenye kompyuta na watu wanayapata kupitia mtandao.

Teknolojia ya habari na mawasiliano imeleta mapinduzi ya hali ya juu katika utoaji wa huduma za maktaba.

Kwa sasa mtumiaji wa maktaba haitaji kutembelea maktaba moja kwa moja kuonana na wakutubi kwa ajili ya kupata machapisho.Huduma ya maktaba mtandaoni itamsaidia kupata machapisho mahali popote na kwa Muda wowote atakapohitaji huduma ya machapisho.

Katika kupata huduma hiyo ni muhimu mtumiaji wa maktaba kuwa na kompyuta na kifaa cha kuruhusu kupata huduma ya mtandao.Iwapo hauna vifaa hivyo ni vizuri ukatembelea ofisi za Posta au mahali penye huduma ya mtandao(Internet cafe shop)


Jackson Chacha

Mkutubi- Chuo cha Uongozi wa  Mahakama 

Email:jackson.chacha@ija.ac.tz


Jumanne, 22 Oktoba 2019

KUNA SIRI ILIYOFICHIKA KATIKA VITABU


Kama vile ambavyo kuna siri katika kupata utajiri,kuwa na ndoa bora;vivyo hivyo kuna siri kubwa iliyojificha katika vitabu.
Jamii imekuwa na mwamko mdogo wa usomaji wa vitabu kwa sababu kadha wa kadha.Lakini sababu mojawapo ambayo inachagiza jamii isiwe na mwamko wa kusoma vitabu imejikita katika tamaduni.
Tamaduni zetu zimeathiri usomaji wa vitabu kuwa duni,Hii inatokana jamii imejikita kushugulika na shughuli za kijamii zaidi kama vile kulima ,kucheza ngoma n.k.
Tunaona asilimia kubwa ya wateja wengi wa maktaba zetu ni wanafunzi na wanavyuo , pia inatoka na kundi hili wanasoma vitabu iwasaidie katika kujibia mitihani yao.

Kwa nini vitabu vimebeba siri?

Kwanza, Kitabu kinafanya msomaji kuwa mbunifu na kupata maarifa mengi yatakayomsaidia  kufikia katika maendeleo ya hali ya juu.Kwa hiyo tunaweza kusema kuna faida kubwa kwa jamii kujijengea tabia ya kusoma vitabu ni chanzo cha kupata maendeleo.

Pili,Kitabu kinasaidia kujenga jamii inayo heshimu haki za binadamu.Tunaona kwa sasa nchi nyingi zinapambana na raia wake kuheshimu haki za binadamu.Nahamini kupitia siri iliyojificha kwenye kitabu itasaidia jamii kuwa utu na kuwajali watu wengine itapunguza visa vinavyotokea vya uvunjifu wa haki za binadamu.

Naomba nihitimishe makala hii kwa kuwahimiza wanajamii kujenga tabia ya kusoma vitabu ili kusaidia jamii zetu ikue kimaendeleo.



Jackson C. Chacha
Lushoto,Tanzania
22/10/2019

Jumamosi, 6 Aprili 2019

KUJENGA JAMII YENYE UELEWA NA HUDUMA ZA KIUKUTUBI

Awali ya yote nitumie ukurasa huu kuwashukuru nyote mnaopitia ukurasa huu kwa ajili ya kujifunza na kupata elimu zinazohusu huduma za Maktaba.karibu sana.
Naomba nianze moja kwa moja kwa kuleta ufafanuzi wa mada tajwa hapo juu.

MKUTUBI ni Nani?
Kwa kweli hili neno linaweza kuwa geni masikioni mwa watu wengi ila ndiyo ukuaji wa kiswahili ulivyo ila itoshe kusema Mkutubi ni mtu mwenye weledi wa taaluma ya maktaba na kazi yake kubwa ni kuweka mpangilio mzuri wa machapisho yote yaliyopo ndani ya maktaba ili kumrahisishia msomaji kupata machapisho kwa urahisi.

Baada ya kufahamu dhana nzima ya neno "Mkutubi" tuangalie lengo la mada yetu.

Kwa ujumla maktaba ni mkusanyiko wa machapisho mbalimbali yaliyopangiliwa kwa usahihi kumrahisishia msomaji aweze kupata hitaji lake kwa muda sahihi.
Maktaba haiwezi kukamilisha kazi zake bila kuwepo Mkutubi aliyepata mafunzo/elimu ya kutosha ya kiukutubi ,ambayo itaweza kukamilisha maana nzima ya uwepo wa huduma ya maktaba.

Jamii ina wajibu wa kuelewa huduma za maktaba ili kuwa na taifa lenye watu walioelemika,hivyo ni jukumu la serikali kuongeza nguvu zaidi kwenye kujenga miundombinu ya kutosha hasa sehemu za pembezoni zizofikika huduma za maktaba kupanua wigo kwa jamii kuelimika.

Jumapili, 15 Januari 2017

KUMJENGEA MTOTO KUWA NA TABIA YA USOMAJI WA VITABU

Usomaji wa vitabu kwa nyakati hizi hauwezi kukwepeka hasa katika ulimwengu huu unaolekea kwenye mapinduzi makubwa ya ukuaji wa sayansi na teknolojia.
'' Shirika la UNESCO linasema utamaduni wa kujisomea vitabu unazidi kupungua duniani. Tanzania ilifikia kiwango cha juu zaidi cha usomaji wa vitabu katika miaka ya 70.''
Tamaduni hii ya usomaji wa vitabu hasa kwa jamii za Kiafrika umekuwa duni sababu ikiwa ni mifumo tuliorithi kutoka kwa wakoloni lakini sababu hizi zisiwe kikwazo za jamii kutosoma vitabu.
Tabia ya kumjengea mtoto kuwa na mazoea ya kusoma vitabu ni njia muhimu sana itakayomsaidia mtoto kuwa na ukuaji ulio bora.
Kwa sasa najua sio tatizo tena kwa wazazi kusoma vitabu vyenye kuleta tija ya maendeleo.

Hatua za kufuata katika kumjengea mtoto tabia za usomaji vitabu
  • Mzazi kuwa mfano wa kuigwa katika kusoma kitabu... weka utaratibu maalumu kwa familia kuwa na programu ya kusoma vitabu.
  • Msaidie mtoto kusoma kitabu hasa sehemu zenye kuleta utata.(zingatia umri na uelewa wa mtoto)
  • Mwekee mtoto utaratibu mzuri wa kusoma kitabu na kuwasilisha taarifa fupi mara amalizapo.
  • Jenga utaratibu wa kumnunulia vitabu mbalimbali hasa vitabu vinavyochochea maarifa kwako na mtoto.
  • Mpongeze mtoto anapoonesha juhudi ya kusoma (Chagua zawadi zinazochochea usomaji)  

         
Hongera sana kwa kutimiza zoezi hili
Soma vitabu upate maarifa kwa sababu maarifa mengi yamefichwa


Kwa maoni na mawasiliano
Clement,Jackson
Librarian - The university of Dodoma (UDOM)
E-mail:jackson.clement81@yahoo.com

Jumatano, 16 Desemba 2015

LIBRARY AND SOCIETY-1

A library is a collection of sources of information and similar resources, made accessible to a defined community for reference or borrowing.[1] It provides physical or digital access to material, and may be a physical building or room, or a virtual space, or both.[2] A library's collection can include books, periodicals, newspapers, manuscripts, films, maps, prints, documents, microform, CDs, cassettes, videotapes, DVDs, Blu-ray Discs, e-books, audiobooks, databases, and other formats. Libraries range in size from a few shelves of books to several million items. In Latin and Greek, the idea of bookcase is represented by Bibliotheca and Bibliothēkē (Greek: βιβλιοθήκη): derivatives of these mean library in many modern languages, e.g. French bibliothèque. The first libraries consisted of archives of the earliest form of writing—the clay tablets in cuneiform script discovered in Sumer, some dating back to 2600 BC. Private or personal libraries made up of written books appeared in classical Greece in the 5th century BC. In the 6th century, at the very close of the Classical period, the great libraries of the Mediterranean world remained those of Constantinople and Alexandria. A library is organized for use and maintained by a public body, an institution, a corporation, or a private individual. Public and institutional collections and services may be intended for use by people who choose not to—or cannot afford to—purchase an extensive collection themselves, who need material no individual can reasonably be expected to have, or who require professional assistance with their research. In addition to providing materials, libraries also provide the services of librarians who are experts at finding and organizing information and at interpreting information needs. Libraries often provide quiet areas for studying, and they also often offer common areas to facilitate group study and collaboration. Libraries often provide public facilities for access to their electronic resources and the Internet. Modern libraries are increasingly being redefined as places to get unrestricted access to information in many formats and from many sources. They are extending services beyond the physical walls of a building, by providing material accessible by electronic means, and by providing the assistance of librarians in navigating and analyzing very large amounts of information with a variety of digital tools.

Jumatatu, 16 Machi 2015

Ongezeko la picha za watoto mitandaoni siyo sahihi

Maendeleo ni matokeo ya jitihada na nguvu zilizotumika katika kuwekeza. Taifa haliwezi kupata maendeleo ya kweli mpaka pale thamani ya watoto wake inapowekwa wazi kwa kila raia.

Mtoto ni rasilimali ambayo ikiandaliwa vyema taifa linaweza kufikia maendeleo na kuondokana na umasikini. Familia, jamii na taifa kwa ujumla tuna wajibu wa kutambua thamani ya watoto, kuwathamini, kuwalinda na kuwapatia haki zao kama elimu. Kufanya hivyo kutakuza vipaji vyao ambavyo baadaye vitakua taaluma.

Jinsi utandawazi unavyozidi kuenea, tumekuwa tukizidi kuona picha za watato wadogo mitandaoni wakiwa watupu bila nguo, wengine wameshika chupa za pombe kana kwamba wanakunywa na wengine wakivuta sigara.Je, hizi picha zinawapa watoto ujumbe gani?

Kama mtoto akifanya kosa mzazi unampiga picha badala ya kumuelekeza, unamfundisha nini? Inakera sana kuona ongezeko la usambazaji wa picha na video za watoto wadogo wakiwa uchi wakifanya ngono.

Jamii itambue kuwa ni kosa la jinai kisheria kurekodi mtoto katika hali yoyote bila idhini ya mzazi au mlezi wake. Vilevile ni kosa la kimaadili na kitaaluma (kwa mpiga picha) kuweka video ya mtoto akiwa mtupu bila kuficha sura yake kwa ajili ya kumlinda mtoto huyu. Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 inatamka wazi kwamba ‘Mtu hatachapisha, kutengeneza, kuonyesha au kuagiza kuchapishwa, kuendeshwa au kuonyeshwa picha au taswira ya mtoto au mtoto aliyefariki, inayoonyesha ukatili au katika pozi za ngono.’ Sheria inatamka kwamba yeyote atakayekiuka masharti ya maelekezo ya kutopiga ama kuchapisha picha za mtoto kama ilivyoelezwa hapo juu, anatenda kosa la jinai na atakapotiwa hatiani atalipa faini isiyopungua shilingi laki tano au kifungo cha miezi sita au vyote kwa pamoja. Ama kwa kujua au kutokujua, jamii hukiuka sheria hii mara nyingi.

Picha hizi hudhalilisha watoto, familia zao na hata kuwaathiri kisaikolojia watoto wenyewe na rafiki zao ambao pia ni watoto.

Haziwasaidii kwa namna yeyote zaidi ya kuharibu heshima na utu wa watoto hawa na kudhoofisha ukuaji na maendeleo yao. Watoto ni kama vioo, wanaakisi kile wanachokiona mbele yao. Wahalifu katika kupiga na kusambaza picha za watoto mitandaoni ni jamii nzima hasa wanaochekelea wakipata picha hizi na wenye mshawawa wa kuzisambaza kwenye makundi yao mitandaoni. Wengine ni wamiliki wa vibanda vya filamu mtaani, maarufu kama ‘vibanda umiza’. Hawa wanaonyesha filamu za aina zote bila kujali umri wa wateja wao. Watoto wadogo wanaruhusiwa kuingia kuona filamu za ngono alimuradi wanazo pesa za kiingilio. Ingawa mzazi huwezi kuwa kila mahala alipo mwanao. Kama jamii na taifa kwa ujumla tunao wajibu wa kuhakikisha tunawakinga watoto na mambo yanayoweza kuhafifisha ukuaji wa vipaji vyao na maendeleo yao.

Ili tuweze kuwekeza kupitia watoto hawana budi kuheshimiwa utu wao. Ni jukumu la jamii nzima kuepuka kusambaza picha za watoto zinazodhalilisha utu wao, jambo ambalo limeenea sana hasa katika mitandao ya kijamii. Kufanya hivyo kunaweza waathiri kisaikolojia, jambo linalodumaza maendeleo yao hata wanapokua watu wazima. Kama jamii na taifa kwa ujumla hatuna budi kuwawekea mazingira mazuri watoto yatakayo imarisha afya zao kimwili na kiakili ili kuandaa taifa la kizalendo litakalowajibika kikamilifu kukua kimaendeleo toka ngazi ya kaya hadi taifa. Wote kwa pamoja hatuna budi kuwapongeza pale wanapofanya vizuri, kuwatia moyo pale wanapokata tamaa kufanya jambo fulani na kuwaelekeza kwa upendo pale wanapokosea na si kuwapiga picha na kuchekelea makosa yao na rafiki zetu.

Makala haya yameandaliwa na wataalamu wa makuzi toka Sema

Source:http://www.mwananchi.co.tz

Jumanne, 10 Machi 2015

TEKNOLOJIA YA KISASA YA UKUSANYAJI WA TAARIFA KUTOKA KAMPUNI YA PUSH OBSERVER

Push Observer Limited ni kampuni ya Tanzania inayomiliki vyombo vya kiinteligencia na teknolojia ya sanaa ya kufuatilia, kukamata na kuchuja vyombo vya habari -magazeti, matangazo (radio & televisheni), Internet na uchambuzi, ripoti ya ushindani kwa ajili ya biashara, serikali na wateja wengineo wa mashirika yasiyo ya kiserikali.

Hivi sasa, Push Observer wanachunguza vituo vya redio 90+, vituo vya televisheni 15+, magazeti (magazeti, majarida, magazeti na majarida) 70+ na machapisho online ikiwa ni pamoja na blogs na mitandao maudhui.

Observer ni kampuni ya kiTanzania inayoongoza kidigitali, kwa viwango vya kimataifa na ushirikiano wa kimataifa katika data na uanachama na vyombo kama FIBEP, Nudge, Vision Critical, na Harvard Innovation Labs. Kwa mujibu wa Mkuu wa Mikakati wa Six Telecoms, Kampuni mama ya Push Observer, Rashid Shamte alisema kuwa kupitia teknologia hii ya usambazaji ya kisasa, wateja wao wataweza kupata habari taarifa muhimu na mpya masaa ishirini na nne ya wiki.

Aliongeza kuwa,tumezindua teknolojia hii kwa wateja wetu kutokana na teknologia ya uchunguzi wa vyombo vya habari kubadilika sana miaka ya karibuni”. “Huduma hii ya kusambaza taarifa imekuwa ya kisasa, rahisi na ya ubora wa hali ya juu kutokana na uwekezaji wetu katika teknolojia hii. Wana vifaa vya kisasa ambavyo vinaweza kupata taarifa kupitia televisheni, magazeti, mitandao ya kijamii na redio kwa muda muafaka, vifaa hivyo vinauwezo wa kupata taarifa had 350,000 kutoka vyombo mbali mbali. Kwa kutambua mahitaji ya wateja wetu kupata habari na taarifa za muhimu tumeamua kuzindua huduma hii na ili kuwahakikishia wateja wetu upatikanaji wa taarifa muhimu na taarifa zinginezo za kwene vyombo vya habari kwa muda muafaka” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Push Observer, Tom Kyalo.